KISWAHILI SANIFU

Bwana Maina Muhindi

Baada ya siku nyingi huko

Afrika Kusini., ameingia London

 

 

CLICK HERE FOR - Methali za kiswahili ---- Swahili proverbs

 

KISWAHILI SANIFU

 
 

METHALI ZA KISWAHILI

1.  Ada ya mja, hunena: muungwana ni kitendo

2.  Adui mpende.

3.  Afua ni mbili, kufa na kupona.

4.  Akomelepo mwenyenji na mgeni koma papo.

5.  Ajali haina kinga.

6.  Aliye juu yu juu.

7.  Aliye kando haangukiwi na mti.

8.  Aliyepeleka mkono kutamalaki si kazi.

9.  Anipendaye nami nampenda, anikataye, napunguwa simanzi.

10. Anipendaye nami nampenda, anitakaye, napunguwa simanzi.

 

 CLICK HERE FOR MORE

 

 

TANAKALI ZA SAUTI

1.   Giza totoro.

2.   Kweupe pepepe.

3.   Kufa fofofo.

4.   Mweusi tititi.

5.   Nyeupe pepepe.

6.   Kunyamaza jii.

7.   Kujaa pomoni.

8.   Kukataa kata kata.

9.   Kutulia tulii.

10. Kunyooka twa.

 

CLICK HERE FOR MORE

 

TAKRIRI

1.   buheri wa afya

2.   balaa na beluwa

3.   dhahiri shahiri

5.   bure bilashi

6.   daima dawamu

7.   miaka na dahari

8.   harusi wala matanga

9.   togo wala jando

10. uso kwa macho

 

CLICK HERE FOR MORE

 

MISEMO

kupiga

kupiga pasi

kupiga domo

kupiga mbizi

kupiga picha

kupiga ngoma

kupiga kelele

kupiga kofi

kupiga simu

kupiga ramli

kupiga kilemba

kupiga kafi

kupiga chafya

kupiga zumari

kupiga miyao

 

CLICK HERE FOR MORE

 

TASHBIHI

1. Kuadimika kama wali wa daku.

2. Kubahatika kama mwana aliyezaliwa Ijumaa.

3. Kubaidika kama ardhi na mbingu.

4. Kudahadari kama mtu anayetoka roho.

5. Kuganda kama kigaga.

6. Kujitia katikati kama mchuzi wa ugali.

7. Kukonda kama ng'onda.

8. Kuwa na miguu mirefu kama korongo.

9. Kuwa na shingo nene kama mbuyu.

10. Kuwa na maneno mengi kama chiriku.

 

SEMI ZA KISWAHILI ( coming soon)

 

JAMAA

ami - kaka yake baba yangu

baba - mzazi wangu wa kiume

baba mkwe - baba yake mke wangu

baba wa kambo - mume wa mama yangu lakini si baba mzazi

babu - baba yake mama

bibi - mama yake mama

binti - mtoto wa kike

dada - mtoto mwanamke wa mama

kaka - mtoto mwanamume wa mama

 

RANGI

mifano

chanikiwiti                                rangi ya samli

kijani                                        rangi ya sneri

kijani kibichi                              rangi ya udongo

waridi                                        rangi ya fedha

majano                                      rangi ya dhahabu

manjano mabichi                        hudhurungi

majano mwangaza                     samawati

 

 

MAJINA YA MAKUNDI

1.  Umati wa watu

2.  Furushi la nguo.

3.   Tita la kuni.

4.   Darasa la wanafunzi.

5.   Koja la maua.

6.   Jozi ya karata.

7.   Kundi la ng'ombe.

8.   Kifungu cha mchanga.

9.   kichaka cha miti.

10. Mkururo wa watoto.

 

 

 WATU MBALI  MBALI

1.   kibogoyo                            - mtu asiyekuwa na meno

2.   bubu                                  - mtu asiyeweza kusema.

3.   kibyongo                            - mtu mwenye nundu mgongoni.

4.   kiwete                                - mtu aliyelemaa miguu.

5.   mja - mzito                         - mwanamke mwenye mimba.

6.   kiguru                                 - mtu mwenye mguu mbovu na anakwenda kwa kuchechemea.

7.   kiziwi                                  - mtu mwenye masikio mabovu asiyeona.

8.   kipofu                                  - mwenye macho mabovu asiyeona.

9.   chongo                                - mtu ambaye jicho lake moja tu ndilo linaloona.

10.  mwenda - wazimu                - mtu asiye na akili timamu. 

 

WAFANYIKAZI

Mfanyakazi                  Kazi

Mchuuzi                      Mtu anayeuza vitu rejareja.

Mfinyanzi                     Mtu anayefanza vyungu na vyombo vingine kwa udongo.

Mganga                       Mtu ajuaye habari za madawa na kuzitumia kuponyesha watu.

Mgema                        Mtu apandaye mnazi kukata karara lake ili kutoa maji yake, yaani tembo.

Mhunzi                        Mfua chuma.

Mjumbe                       Mtu aliyetumwa.

Mkalimani                    Mtu aelezaye maneno ya lugha moja kwa lugha nyingine kwa kusema, si 

                                   kwa kuandika.

Mwezekaji                    Fundi wa kuezeka nyumba.

Mwizi                           Mtu aibaye, achukuaye vitu vya watu bila ya ruhusa.

Muuguzi                       Mtunzaji wagonjwa.

 

VYOMBO

kasiki                                  mtungi

gudulia                                sufuria

chungu                                karai

legeni                                  sinia

sahani                                 bakuli

bilauri                                  buli

birika                                   debe

chano                                  ungo

kikango                                kandili

kibatari                                 chupa

susu                                     pakacha

kikapu                                  gunia

kasha                                   sanduku

tasa                                      mkoba

mfuko                                    ala

kata                                       pipa

kikombe                                 seredani

tanuri                                     kisima

kidawa                                   kibeti                           kabati

 

 

MASHAIRI

1. FITINA

Mara nyingi, sisi binadamu twatumbukia kwenye mtumbwi wa mfinyanzi na kubanwa na biwi la simanzi kwa msiba wa kujitakia wenyewe. Ni dhahiri shahiri ya kwamba baadhi yetu ni vibilifitina na kina pangu pakavu tia mchuzi. Mara kwa mara, twahatarisha maisha ya ndugu zetu kwa kuwaonea wivu na kuwafitini bure.

Ndiposa leo hii najibwaga katika ukumbi huu wa sanaa kwa kurejelea shairi murua la msanii
Rwechungura. Tafadhali jumuika nami na ulisome kwa fahamu na sina shaka utafaidi.

Bwana Muhindi.

                      FITINA

Fitina mtu khatari, siwezi kukhadithia,
Mzushi hana nadhari, mjasusi wa kuzua,
Anuka kama jodari, papa bovu la India,
  Fitina mvunja mji, umwonapo tahadhari.

Fitina hana jeuri,  usoni huchekelea,
Hudai hana kiburi, laghai kunyenyekea,
Hujifanya yu tayari, kitini kukwinukia,
  Fitina mvunja mji, umwonapo tahadhari.

Fitina mtu ayari, heshi kukutembelea,
Si mwema na si mzuri, hakai akatulia,
Upole akuvinjari, apate kukuzulia,
  Fitina mvunja mji, umwonapo tahadhari.

Fitina mfano ngiri, heshima hajatambua,
Domo halitaghairi, kutoa yasio njia,
Hata awe mshairi, fitina wote sawia,
  Fitina mvunja mji, umwonapo tahadhari.

Fitina hana bahiri, maneno kupangilia,
Fitina hana dosari, zaidi ya laki mia,
Fitina katika pori, hukaa akangojea,
  Fitina mvunja mji, umwonapo tahadhari.

Fitina si urafiki, ni utovu wa tabia,
Halimukhusu fikiri, kwa nini kushikilia,
Na kufanya dhamiri, kukaa kusimulia,
  Fitina mvunja mji, umwonapo tahadhari.

Fitina khasa kafiri, karibu mwenye kuua,
Huzikusanya khabari, kila pembe ya dunia,
Uulizapo hakiri, adui wa watu pia,
  Fitina mvunja mji, umwonapo tahadhari.

Fitina leo kariri, usome ukirudia,
Ndoa ikisha shamiri, huwezi kuitangua,
Ila atake Kahari, wakati ukiwadia,
  Fitina mvunja mji, umwonapo tahadhari.

Fitina hii nadhiri, siku moja tatimia,
kugundua ikijiri, kifungo nitachukua,
Fitina hata tajiri, ras yake taitoa,
  Fitina mvunja mji, umwonapo tahadhari.

 

 

INSHA / HADITHI ZA KUBUNI (soon)

 

VITENDAWILI ( soon)

 

MASWALI  NA MAJIBU (soon)